Wednesday, July 1, 2015

WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO 2015/2016

Ofisi ya Waziri Mkuu - TAMISEMI imetangaza majina ya wanafunzi waliochaguliwa
kujiunga na Kidato cha Tano na Vyuo vya Ufundi kwa mwaka 2015.
Wanafunzi waliochaguliwa ni kutoka shule za Serikali na zisizo za Serikali.
Jumla ya wanafunzi 55,003 wakiwemo wasichana 23,303 na wavulana 31,700 wamechaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano na Vyuo vya Ufundi.
Kati ya wanafunzi waliochaguliwa 29,744 wakiwemo wasichana 11,450 na wavulana 18,294 sawa na asilimia 54.08 watajiunga na masomo ya Sayansi na Hisabati; na wanafunzi 25,259 wakiwemo wasichana 11,853 na wavulana 13,406 sawa na asilimia 45.92 wamechaguliwa kusoma masomo
ya Sanaa na Biashara.

Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na shule ya sekondari Mkuu ni 279, wakiwemo Wasichana 138 na wavulana 141. Wanafunzi hao wamepangwa katika tahasusi za HGK, HGL, HGE, EGM, CBG, PCB na PCM.

Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano mwaka 2015 wataanza muhula wa kwanza tarehe 18 Julai, 2015 na hakutakuwa na fursa ya mabadiliko yoyote ya shule. Wanafunzi wote wanatakiwa kuripoti katika shule walizopangwa kwa wakati. Endapo mwanafunzi atachelewa kuripoti kwa zaidi ya siku 14 kuanzia tarehe ya mwisho ya kuripoti, nafasi yake itachukuliwa na mwanafunzi mwingine aliyekosa nafasi.

Orodha ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano na Vyuo vya Ufundi mwaka 2015 inapatikana kwenye tovuti ya OWM-TAMISEMI ya www.pmoralg.go.tz

KUPATA JOIN-INSTRUCTION,   >>>BONYEZA HAPA<<< kwa microsoft word.


KUPATA JOIN-INSTRUCTION,   >>>BONYEZA HAPA<<< kwa PDF



Imetolewa na Ofisi ya Taaluma
Shule ya sekondari Mkuu

7 comments:

  1. NAOMBA LINK YA SELECTION ZA F.V 2016 AMBAYO INA MAJINA YAKIWA KWENYE PDF FORMAT.
    NAHAHA NI BALAA KWANI NI NGUMU KUWAPATA WALIOCHAGULIWA KUJA SHULENI KWANGU.
    INAITWA "NANGA" IKO IGUNGA TBR.
    BY MTAALUMA MWENZAKO

    ReplyDelete
    Replies
    1. Nimeshaweka Post yenye Link kwa PDF, tembelea post hiyo mpya udownload. Na pia nimekutumia kwa email yako.

      Asante kwa kutembelea blog yetu.

      Delete
  2. TEMBELEA HII LINK...

    https://docs.google.com/uc?export=download&id=0B-3NPtAZatF3UHc2b2daV21ldGZ3TUxINHZKeVZEdmhXSG9N

    NIMEKUWEKEA YA SHULE YAKO. KAMA ITAKUSUMBUA KUDOWNLOAD TAFADHALI NICHEK KWA EMAIL mkuutaaluma@gmail.com au mrtarimo@outlook.com

    ReplyDelete
  3. https://docs.google.com/uc?export=download&id=0B-3NPtAZatF3UHc2b2daV21ldGZ3TUxINHZKeVZEdmhXSG9N

    COPY HIYO LINK HAPO JUU KAMA ILIVYO THEN PASTE IT KATIKA ADDRESS BAR YA BROWSER YAKO (napendekeza mozilla firefox) THEN ITAKULETEA OPTION YA KUDOWNLOAD SHULE YA NANGA SEC WALIOCHAGULIWA. IPO KATIKA EXCEL. UKIFANIKIWA TAFADHALI NIJULISHE.

    ReplyDelete
  4. Upo vizuri Mtaaluma wa Mkuu Sec... kuna ishu kama hiyo nimekutumia kwa email yako tafadhali na mm nisaidie nipate ya shule yangu... Naomba maana nimejaribu kuchambua nikashindwa.

    ReplyDelete
  5. Naomba nisaidue link ya kuchen walio chaguliwa awamu ya pula shule ya itilima ya simiyu

    ReplyDelete
    Replies
    1. Naona Admin kawa kimya, labda nikusaidie kama hutojali bwana Nassoro...

      Tumia link ilotolewa hapo kwenye ukurasa wa kwanza wakati unafungua blog hiina utaona post ya waliochaguliwa second selection 2016
      au tumia hii: http://tamisemi.go.tz/form_five_selection/second/
      au tembelea website ya TAMISEMI www.tamisemi.go.tz

      Delete