JOIN INSTRUCTIONS

MAAGIZO YA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI MKUU

UTANGULIZI:

Shule ya Sekondari Mkuu ni shule nzuri ambayo ni mchanganyiko kuanzia Kidato cha I – IV. Wanafunzi wa kidato cha tano na sita ni wasichana tu.
Wanafunzi wote wasichana wa kidato cha tano na sita wanakaa kwenye mabweni yaliyopo shuleni. Wanafunzi wa kidato cha 1 - 4 wanalala nyumbani.
Shule  ya Sekondari Mkuu iko katika mazingira mazuri ya mwanafunzi kusoma na kuweza kufaulu vizuri kama ataonyesha bidii ya kusoma. Shule inao walimu wa kutosha na huduma zote muhimu kwa wanafunzi zipo shuleni. Mwanao aitumie nafasi hii aliyopewa na Serikali vizuri baadaye alisaidie Taifa letu, wazazi wake na yeye mwenyewe kwa siku za baadaye akizingatia kwamba wenzake wengi hawakuchaguliwa.
Kwa ushindi huo wa mwanao tunawapongeza  wewe mzazi pamoja na mwanao kwa kuchaguliwa kwake.


USAFIRI WA KUJA SHULENI

Mwanafunzi akifika moshi mjini stendi kuu ya mabasi akitokea popote pale, uliza na apande magari yaendayo Rombo kupitia Mwika hadi Tarakea. Shule yetu ipo umbali wa kilomita 60 kutoka Moshi mjini hadi Mkuu Rombo kabla hujafika Tarakea. Nauli ya kutoka Moshi mjini hadi Mkuu Rombo ni Tshs. 4000/= hadi Tshs. 5000 kutategemeana na gari. Kwa wanafunzi wanaotoka Dar es Salaam au kupitia DSM wapande magari ya  Dar express, Meridian, Esther coach, Saibaba, Metro coach, Tilisho Coach yanayokuja moja kwa moja Rombo. Kwa Kutokea Dodoma panda bus la Shabibi  au Ngasere linalokuja moja kwa moja Rombo. Wanaotokea Singida panda bus la Mtei Express la Rombo. Na kutokea Mwanza panda bus la Mghamba.

KITUO CHA KUTEREMKIA

Ukitokea Moshi mjini mwambie kondakta wa gari utateremkia Mkuu-Kanisani vilevile kwa wale wanaotokea Tarakea kuelekea Moshi nao watateremkia Mkuu-kanisani. Kutoka hapo Mkuu-Kanisani kuelekea shuleni ni umbali wa mita 150 utakuwa umefika shuleni.
Ukifika shuleni utaripoti na kupokelewa na mwalimu wa zamu au Makamu wa Mkuu wa shule ambao wote watakuwepo shuleni kwa kipindi hicho. Baada ya kuripoti shuleni utasajiliwa ofisini kwa Makamu wa Mkuu wa shule ukiwa na mahitaji yote muhimu uliyoagizwa kuleta shuleni.


HUDUMA ZINAZOPATIKANA SHULENI

Shule inalo duka ambalo hutoa huduma za mahitaji karibu yote muhimu kwa wanafunzi na watumishi wote wa shule. zahanati ya Mission Mkuu iko karibu na shule. Hospitali kubwa ya Wilaya ipo karibu na shule ina gari, usafiri wa kuja shuleni na kurudi nyumbani ni mzuri kwani shule ipo karibu sana na barabara, Benki, Posta vyote viko karibu.


MIRADI YA SHULE:

Shule yetu inayo miradi kama ifuatayo ambayo huhudumiwa na wanafunzi na baadhi ya watumishi ambao vile vile hutumika kwa mafunzo:-

1.    Duka la shule
2.    Ng’ombe wa maziwa
3.    Bustani ya mboga
4.    Mgahawa
5.    Shamba la migomba


Kwa maelezo zaidi kuhusu tarehe ya kuripoti shuleni, ada na michango ya shule, uniform, na form mbalimbali zinazoambatana na join-instructions, bonyeza Link hizo hapo chini kwa form 1 au form 5.


Download>>>FORM ONE 2024 Joining Instuctions



Download>>>FORM FIVE 2024/2025 Joining Instructions





Mwisho tunampongeza tena mwanao kwa kuchaguliwa kwake na tunamkaribisha

Shule ya Sekondari Mkuu.

KARIBU SANA.

 

50 comments:

  1. Kazi nzuri sana, mmekuwa wa kisasa, keep it up

    ReplyDelete
  2. Enter your comment...hakuna bwen kwa boys

    ReplyDelete
    Replies
    1. Kama ilivyoelezwa hapo juu. Kwa O-level wanafunzi ni wa kutwa. Na kwa A-level wanafunzi ni wa bweni tena wakike tu!

      Vilevile kwa O-level kuna private hostel za kike na kiume zinazomilikiwa na kanisa (parokia ya Mkuu).

      Delete
  3. ninaomba msaada wa taratibu za kumleta mtoto O-level. nimekuwa interested sana na namna shule inafanya vizuri na ipo kisasa katika huduma zake.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Shule hii ni ya serikali. Wanafunzi hupangiwa hapa na serikali. Ukitaka kumleta mwanao ambaye hajapangiwa hapa itakubidi kufuata taratibu za uhamisho wa mwanafunzi...

      Delete
  4. Asante kwa maelekezo mazuri na ushauri 1. naweza kupata namna ya mawasianiano na ofisi ya taaluma kama kujua nafasi kama zipo na taratibu hizo za kuhamisha mtoto?. naomba msaada tafadhali.

    ReplyDelete
  5. Namba za uongozi wa shule tembelea link hii:
    https://mkuutaaluma.blogspot.com/p/contact-us.html

    ReplyDelete
  6. Sorry, the page you were looking for in this blog does not exist. Mine coins - make money: http://bit.ly/money_crypto

    Mine coins - make money: http://bit.ly/money_crypto


    najibiwa hivyo. But shida yangu kubwa ni kufahamu kama nafasi zipo na naweza kufanya utaratibu wa kumleta mtoto

    ReplyDelete
  7. Je hapo shuleni unaruhusiwa kubadili combination Kama una qualifications?

    ReplyDelete
    Replies
    1. Ndio. Tofauti na kuwa na vigezo, pia itategemea na maelekezo yatakayotolewa mwaka huu kuhusu kubadili Comb.

      Delete
    2. Kuna na fasi kwa walewakurudia mtiani wa form four

      Delete
  8. Hongera mkuu secondary kwa kutoa huduma nzuri

    ReplyDelete
  9. Joining instruction ya mwaka huu kwa form five iko tayari?

    ReplyDelete
    Replies
    1. Ndio, ipo tayari. waweza kudownload kwa kupitia link iliyopo hapo juu.

      Delete
    2. Hizo private hostel za kanisa naelewa ni za kulipia. Ningeomba kujua no sh ngapi?je mwanafunzi wa A level anaruhusiwa kutumia

      Delete
    3. Ni kwa ajili ya wanafunzi wa kidato cha kwanza hadi cha nne. Wanafunzi wa kidato cha 5 na 6 wanalala bweni la shule.
      Gharama za hostel ya kanisa ni 600,000 kwa mwaka.

      Delete
  10. Herini sana kwa mwaka mpya na hongereni kwa kazi nzuri mnayofanya hapo.
    Tafadhali naomba kuuliza swali.Wanafuzi waliokuwa kidato cha pili wanaotarajiwa kuingia kidato cha tatu mwaka huu 2021 ni categories gani zinaendelea wakati matokeo bado hayajatoka?Je wanaendelea kuja shuleni au kuna uaratibu mwingine uliotolewa wa kusubiri matokeo ya kidato cha pili yatoke?maana watu wamekuwa njia panda kuhusu matokeo kutotolewa kwa wakati.
    Ninatumaini mtakuwa na fununu juu ya hili japo haijawekwa wazi kama matokeo yatatoka lini!Otherwise mkute mliwapa taarifa kama wasubirie matokeo yakishatoka ndio waende shule.Asante sana naomba kuwasilisha.

    ReplyDelete
  11. Tunaomba joinning instaction za mwaka huu

    ReplyDelete
  12. joining instruction za form5 mwaka huu mbn hazipo online

    ReplyDelete
  13. Tuwekeeni join instruction ya form Five ya 2021

    ReplyDelete
  14. Zipo. Jaribu kudownload tena. Wameshaweka.

    ReplyDelete
  15. Meanangu nataka nimwamishie hapo naomba utararatibu na namba za muhusika ili anielekeze jinsi nitakavyo fatilia uhamisho prem no na vitu vingine ataanza kidato Cha kwanza 2022

    ReplyDelete
    Replies
    1. https://mkuutaaluma.blogspot.com/p/contact-us.html

      Delete
    2. Naomba form za kujiunga form 5 2022/2023

      Delete
  16. Form za kujiunga na form 5 tayari?

    ReplyDelete
  17. Mwisho was tarehe ya kuripoti ni lini?

    ReplyDelete
  18. Mwisho wa tarehe ya kuripoti ni lini?

    ReplyDelete
  19. Ok yumeielewa je? Gorm zinajzwa shuleni au uku nyumbn

    ReplyDelete
  20. Tumeelewa vizur je? Form inatakiwa kujazwa shulen.au nyumbn

    ReplyDelete
    Replies
    1. Mwanafunzi anapaswa kuriport akiwa na form iliyojazwa kikamilifu.

      Delete
  21. Waaoon wonderful I like my schol

    ReplyDelete
  22. Hongereni Mkuu Sekondari Kwa kazi nzuri ya utoaji elimu Kwa vijana wa kitanzania. Naomba kufahamu Kuna huduma ya bweni Kwa o-level both girls and boys Kwa mwaka 2023?

    ReplyDelete
    Replies
    1. Asante. Hakuna huduma ya bweni kwa O-Level. Ila kuna huduma ya hostel binafsi inayotolewa na Parokia ya Mkuu kwa wanafunzi wa O-level wanaotaka kukaa hostel.

      Delete
  23. Je mnapokea wanafunzi wanaohamia

    ReplyDelete
  24. Join instructions za mwaka huu zipo tayari!??

    ReplyDelete
    Replies
    1. Habari? Join instructions zipo tayari. Bonyeza link hapo juu.

      Delete
  25. Mkuu secondary school

    ReplyDelete
  26. Habari, naomba utaratibu namna ya kupata hizo hostel za parokia Kwa wanafunzi wa o level, ikiwezekana na mawasiliano Yao pia

    ReplyDelete
  27. Samahani naomba kuuliza nitapata nafasi ya mwanafunzi wa kidato cha tano anasomea HGK naombeni mnisaidie

    ReplyDelete
  28. nauliza maksi za wasichana join form 5 ni ngapi

    ReplyDelete
  29. Wanafunzi wanasuka au wananyoa wa A level kwenye join instructions akuna about that

    ReplyDelete
    Replies
    1. Soma ukurasa wa tano, kipengele cha Vi.

      Delete