UCHAGUZI WA WANAFUNZI KIDATO CHA TANO 2014 AWAMU YA PILI PAMOJA NA JOIN INSTRUCTION ZA WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI MKUU
Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa imetangaza majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano 2014 awamu ya pili.
Wanafunzi 8,101 wamechaguliwa kujiunga na kidato cha tano awamu ya pili 2014,
kati ya hao 4,987 wamepangwa tahasusi za sayansi ya jamii na biashara na wanafunzi 3,114 wamepangwa tahasusi za sayansi.
Aidha wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na shule ya sekondari Mkuu ni wanafunzi 30, ikiwemo kati yao wanafunzi 6 ni wasichana, na 24 ni wavulana.
Wanafunzi hao wamechaguliwa kusoma tahasusi mbalimbali za Sayansi ya jamii (yaani HGK, HGL, HGE, EGM) na sayansi asilia (yaani PCM, PCB, CBG)
Wanafunzi hawa wanatakiwa kuripoti kwenye shule walizopangiwa kuanzia tarehe 01 Septemba, 2014 na mwisho wa kuripoti ni tarehe 15 Septemba, 2014.
au
Imetolewa na Mtaaluma Mwandamizi
OFISI YA TAALUMA - SHULE YA SEKONDARI MKUU
31/08/2014