Monday, September 1, 2014

SECOND SELECTION KIDATO CHA TANO 2014

UCHAGUZI WA WANAFUNZI KIDATO CHA TANO 2014 AWAMU YA PILI PAMOJA NA JOIN INSTRUCTION ZA WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA SHULE YA SEKONDARI MKUU
Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa imetangaza majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano 2014 awamu ya pili.
Wanafunzi  8,101  wamechaguliwa  kujiunga  na  kidato  cha  tano awamu  ya  pili  2014,
kati  ya hao  4,987  wamepangwa  tahasusi  za sayansi  ya  jamii  na  biashara  na  wanafunzi  3,114 wamepangwa tahasusi za sayansi.

Aidha wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na shule ya sekondari Mkuu ni wanafunzi 30, ikiwemo kati yao wanafunzi 6 ni wasichana, na 24 ni wavulana. 
Wanafunzi hao wamechaguliwa kusoma tahasusi mbalimbali za Sayansi ya jamii (yaani HGK, HGL, HGE, EGM) na sayansi asilia (yaani PCM, PCB, CBG)
Wanafunzi  hawa  wanatakiwa  kuripoti  kwenye  shule walizopangiwa  kuanzia  tarehe  01 Septemba,  2014  na  mwisho  wa kuripoti ni tarehe 15 Septemba, 2014.


au





Imetolewa na Mtaaluma Mwandamizi
OFISI YA TAALUMA - SHULE YA SEKONDARI MKUU
31/08/2014